Posts

Showing posts from April, 2022

Mhe Gekul awataka watanzania kutumia fursa za Royal Tour

Image
  Na. John Mapepele Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Philipo Gekul (Mb) amewataka watanzania  kutumia  fursa iliyotengenezwa  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan   kwenye Filamu ya Royal Tour. Mhe. Gekul ameyasema  haya leo Aprili 29, 2022 kwenye  semina ya wadau wa sekta ya filamu ya Royal Tour katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam. Naibu  Waziri Gekul amesisitiza kuwa Serikali Serikali ipo tayari kushirikiana na wanatasnia ya filamu katika kuendeleza Sekta ya filamu nchini ikiwa ni pamoja na kutengeneza mazingira rafiki na wezeshi yatakayo wawezesha wanatasnia wa ndani na nje ya nchi kufanya shughuli zao nchini. Aidha, amesema yapo maeneo  kadhaa muhimu ambayo Tanzania inaweza kushirikiana na Marekani katika filamu na ikanufaika nayo. Ameyataja maeneo hayo  kuwa ni pamoja  na utayarishaji wa filamu kwa kutumia mandhari zinazo pat...

Mhe Mchengerwa awaongoza wanarufiji kumwombea Dua, Rais Samia

Image
  Na John Mapepele Mamia ya wananchi wa Jimbo la Rufiji leo Aprili 29,2022 wamefanya dua maalum ya kumwombea  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe Samia Suluhu kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa katika eneo la Ikwiriri Wilayani Rufiji. Dua hiyo maalum  imeongozwa na Shehe Athmani  Shabani Bofu  kutoka Utete akishirikiana na mashehe mbalimbali wa Mkoa wa Pwani ambapo wamemwombea kwa Mwenyezi Mungu, Mhe. Rais Samia afya njema na ufanisi kwenye kazi zake za kila siku.  Akiongea kwenye tukio hilo Mhe. Mchengerwa amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais kwa kazi kubwa anayowafanyia wananchi wa Tanzania ikiwa ni pamoja na wananchi wa Rufiji. Amesema wananchi wa Rufiji wamenufaika kwa  kiasi kikubwa na Maendeleo yanayoletwa  na Serikali na  kuwataka kuendelea kushirikiana na Serikali yao ili kujiletea maendeleo zaidi.  Ametaja baadhi  ya maende...

Mhe. Mchengerwa atoa maneno mazito kwa wachezaji wa Simba masaa machache kabla ya kucheza na Orlando leo

Image
  Na. John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa leo Aprili  24, 2022 amezungumza na wachezaji wa Timu ya Simba  masaa machache kabla ya kuingia kwenye mechi ya  marudiano na Orlando Pirates katika mashindano ya kombe la Shirikisho barani Afrika na kuwatakia kila la heri katika mchezo huo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan. Mhe. Mchengerwa ameongea na wachezaji wa Simba kupitia simu ya Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ambapo ametaka  wachezaji kucheza  kwa moyo huku wakitambua kuwa ushindi wa Simba  leo  utaiweka Tanzania  katika ramani ya Afrika ya nchi zenye vilabu vinavyofanya vizuri.  Aidha, ameongeza kuwa  watanzania  na Serikali ipo bega kwa bega na timu hiyo na kwamba wazingatie zaidi mchezo na wapuuze baadhi ya maneno  kuhusu mambo ya usalama kwakuwa  watanzania na waafrika kusini ni ndugu na marafiki na mchezo siyo uadui. " M...

Waziri Mchengerwa atoa siku tatu kwa Bodi ya Filamu Tanzania kutekeleza maelekezo yake

Image
  Na. John Mapepele  Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Mohamed Mchengerwa leo Aprili 23, 2022 amefanya ziara ya kikazi kwenye taasisi ya Bodi ya Filamu nchini (TFB) na kujadili mikakati mbalimbali ya kuboresha na kuleta mapinduzi kwenye tasnia Filamu nchini ambapo ametoa siku tatu za kufanyia kazi maelekezo kadhaa aliyoyatoa.  Mhe. Mchengerwa amesema tasnia ya filamu inazalisha ajira na kutoa mchango mkubwa kwenye taifa hivyoTFB inatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia weledi na kasi ili kuleta mapinduzi yanayositahili kwenye sekta hiyo hapa nchini. Akiwakilisha baadhi ya mikakati ya TFB, kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo,     Mtendaji Mkuu wa Taasisis hiyo, Dkt. Kilonzo Kiagho amesema taasisi hiyo imejiwekea mikakati kabambe ambayo inaendana na miongozo mbalimbali ya Serikali ikiwa ni pamoja na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.  Ameitaja baadhi ya mikakati itakayoleta mageuzi makubwa kwenye tasnia hiyo kuwa ni pamoja na kuanzisha tozo la filam...

Mhe. Mchengerwa akutana na Wawekezaji wa Miundombinu ya Michezo

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa leo Aprili 22, 2022 ameshiriki futari maalum jijini Dar es Salaam. Futari  hiyo maalum imeandaliwa na Ubalozi wa Saudi Arabia na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali. Katika futari hiyo maalum wageni waliohudhuria wameaswa kutenda mattendo mema  katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani na baada ya hapo kama ilivyoelekezwa kwenye kitabu kitakatifu cha Qur'an.

Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa leo Aprili 22, 2022 ameshiriki futari maalum jijini Dar es Salaam. Futari hiyo maalum imeandaliwa na Ubalozi wa Saudi Arabia na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali. Katika futari hiyo maalum wageni waliohudhuria wameaswa kutenda mattendo mema katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani na baada ya hapo kama ilivyoelekezwa kwenye kitabu kitakatifu cha Qur'an.

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa leo Aprili 22, 2022 ameshiriki futari maalum jijini Dar es Salaam. Futari  hiyo maalum imeandaliwa na Ubalozi wa Saudi Arabia na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali. Katika futari hiyo maalum wageni waliohudhuria wameaswa kutenda mattendo mema  katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani na baada ya hapo kama ilivyoelekezwa kwenye kitabu kitakatifu cha Qur'an.

Nendeni mkaishangilie Simba, Afrika Kusini ni salama- Mhe Mchengerwa

Image
  Na. John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Mohamed Mchengerwa amewatoa hofu  mashabiki  wa soka wanaotaka kwenda Afrika Kusini kuishangilia Timu ya Simba katika mchezo wa raundi ya pili robo fainali ya Mashindano ya Kombe la Shirikisho  barani Afrika kuwa watakuwa salama. Mhe. Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo Aprili 21, 2022 kwenye Uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam alipokuwa akiongea na Vyombo vya Habari. "Niseme tu kwamba sisi kama Serikali tunafuatilia  kwa karibu usalama wa timu na hivi ninavyoongea nimemteua Msaidizi wangu Mkurugenzi wa Michezo ili aweze kuniwakilisha kusimamia hili" amefafanua Mhe. Mchengerwa Aidha, Mhe. Mchengerwa amesema watanzania na waafrika Kusini ni ndugu wa muda mrefu hivyo ni mategemeo kuwa  hakutakuwa na jambo lolote linaloweza kuhatarisha usalama.  Ameeleza kuwa  katika mechi hiyo Timu ya Simba inakwenda kushindana  siyo kushiriki ili kuliwakilisha taifa  ambapo amewataka wache...

Kinana aipongeza Wizara kwa kuhifadhi Utamaduni wa Ukombozi wa Bara la Afrika

Mh. Mchengerwa azindua Bodi ya BMT, atema cheche, aitwisha mambo matatu

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa ameitaka Bodi ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) aliyoiteua hivi karibuni, kuifanya michezo nchini kuwa biashara badala ya kuendelea na mazoea ili kutoa ajira na kuchangia kwenye uchumi wa nchi. Mhe. Mchengerwa ameyasema haya leo Aprili 20, 2022 kwenye Ukumbi wa Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam wakati aikizindua rasmi Bodi hiyo ya 15 ya BMT ambapo amefafanua kuwa kazi kubwa ya Bodi hiyo ni kuisaidia Serikali kuandaa timu bora za taifa katika michezo mbalimbali ili ziendelee kufanya vizuri katika michezo kimataifa. Ameitakia Bodi hiyo kuwa na mikakati kabambe ya kuwashirikisha wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali kuja kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo ili kuhakikisha kuwa michezo inapiga hatua. Aidha, Mhe. Mchengerwa ameiagiza Bodi  mambo mahususi matatu ili kuendeleza michezo nchini huku akisisitiza  kuwa mwamko uliopo  leo kwenye  michezo ni maono na Jitihada zil...

Wadau wekezeni kwenye miundombinu ya michezo - Mhe, Mchengerwa

Image
  Na. John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe. Mohamed Mchengerwa amemwakilisha, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Kassim  Majaliwa Majaliwa kwenye ufunguzi wa maabara ya kisasa ya Komputa iliyojengwa kwa ufadhili wa klabu ya Baseball Dodgers ya Marekani kupitia Chama cha Mchezo wa Baseball/Softball Tanzania. Tukio hilo amelifanya leo, Aprili 19, 2022 kwenye Shule ya Sekondari ya Azania jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa taasisi za michezo wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara  Saidi Yakubu na wadau mbalimbali. Mhe. Mchengerwa ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa michezo kujitokeza kuwekeza katika miundombinu ili sekta ya michezo iweze kusonga mbele Ameongeza kuwa dhamira ya Serikali  ni kuendelea kukuza sekta ya Michezo na Sanaa kwa kushikiana na wadau wenye utashi wa kuwekeza katika sekta hizo. "Mpango wa Serikali ni kufanya michezo iwe biashara".ameongeza  Mhe, Mchengerwa Aidha, amesema tayari Serikali imeweka mazingir...

Hongereni Simba- Mhe, Mchengerwa

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa ameipongeza timu ya  Simba kwa ushindi wa  goli 1-0 dhidi timu ya Orlando Pirates Aprili 17, 2022 kwenye dimba la  Mkapa  jijini Dar es Salaam. Pongezi hizi ameendelea kuzitoa leo baada ya zile alizotoa jana mara baada ya kumalizika kwa mechi hiyo. Ikumbukwe kuwa Mhe. Mchengerwa jana aliwaongoza maelfu ya  watanzania kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe Samia Suluhu Hassan kuishangilia Simba katika uwanja wa Mkapa hatimaye ikatwaa ubingwa huo. Asubuhi kabla ya mechi hiyo, Mhe. Mchengerwa baada ya kumaliza kushiriki mashindano makubwa  ya Qur'an barani Afrika  yaliyofanyika kwenye uwanja huo huo wa Mkapa, akiambatana na Naibu Katibu Mkuu  wake Said Yakubu alitoa wito kwa watanzania kujitokeza kuja kuishangilia Simba katika mechi hiyo iliyochezwa kuanzia  saa moja usiku ili ishinde. Ubingwa wa Simba ulipatikana kupitia kwa beki kisiki Sho...

Mhe Mchengerwa atoa wito kwa wananchi kushiriki sensa, anuani za makazi

Image
  Na. John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Rufiji. Mhe, Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa wananchi nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye mazoezi ya kitaifa ya uandikishaji wa anuani ya makazi na sensa yanayoendelea hivi sasa nchini kwa ajili ya maendeleo ya taifa. Mhe, Mchengerwa ameyasema haya leo wakati akiongea na wananchi wa vijiji vya Mgomba, Ngorongo na Kilimani kwenye Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Amefafanua kwamba  mazoezi haya yana faida kubwa kwa nchi yetu  kwa kuwa yanasaidia kupanga  mipango mbalimbali ya maendeleo kwa muda wa sasa  na baadaye. Aidha, ameishukuru Serikali   ya awamu ya sita kwa kukamilisha mipango ya maendeleo katika kipindi kifupi. Ametaja baadhi ya mipango ambayo inatekelezwa kuwa ni pamoja na  miundombinu ya barabara, shule na vituo vya afya na jengo la kujifungulia akina mama ambapo amewataka wananchi kutumia na kusimamia vizuri raslimali zinazotolewa. Aidha ameipongeza...

Maafisa Michezo simamieni vikundi vya mazoezi- Mchengerwa

Image
  Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amewaagiza maafisa michezo nchi nzima kuvisajili vikundi vyote vya mbio za hisani (Marathon) katika wilaya zao na kuvifuatilia ili kutoa motisha kwa vikundi vinavyofanya vizuri na  kuwaandaa wanariadha  kushiriki mashindano ya kimataifa na kusaidia kuzuia maradhi mbalimbali. Mhe, Mchengerwa ametoa agizo hilo leo, Aprili 10, 2022 wakati akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza mbio za hisani kwa ajili ya utoaji wa elimu na ufahamu kuhusu usonji zilizo andaliwa na taasisi ya Usonji ya Lukiza. Ameongeza kuwa wanariadha hao bora watakaopatikana kupitia mbio mbalimbali watashiriki mashindano ya kimataifa na kuliletea taifa medali mbalimbali. Akizungumzia mashindano ya Jumuiya ya madola, Waziri Mchengerwa amesema washiriki wote watakao kwenda kushiriki katika michezo hiyo Serikali inawahudumia, na wote wapo kambini wakiendelea kujiandaa vyema kuwakabili washindani wao katika m...