Posts

Showing posts from September, 2020
Image
  Ivan Edmund kutoka kampuni ya dawa za binadamu ya Philips Pharmaceuticals Tanzania Ltd. akitoa dawa kwa mwananchi aliyekutwa na tatizo la  moyo  mara baada ya kupata matibabu wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo Duniani yaliyofanyika jana katika viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Katika maadhimisho hayo wananchi walipata bila malipo huduma za Upimaji,ushauri, matibabu ya moyo na rufaa ya moja kwa moja kwa wale waliokutwa na matatizo ya moyo yaliyohitaji matibabu ya kibingwa. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akitoa elimu ya jinsi gani unaweza kuepuka kupata magonjwa ya moyo kwa wananchi waliofika katika viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo wilya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo Duniani. Katika maadhimisho hayo wananchi walipata bila malipo huduma  za Upimaji,ushauri, matibabu ya moyo na rufaa ya moja kwa moja kwa wale wali...

UN yamuunga mkono Magufuli kutokomeza ukatili wa mwanamke Ikungi

Image
                                       Picha ya pamoja ya Mkuu wa mkoa wa Singida  Dk. Rehema Nchimbi(mwenye kilemba) na  wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na wadau mbalimbali wa maendeleo mara baada ya uzinduzi wa mradi Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Rehema Nchimbi(kulia) akiwa na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania, Zlatan Milisic baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi    Na John Mapepele, Ikungi  MKUU wa  Mkoa wa Singida Mhe, Dk. Rehema Nchimbi  leo amezindua  miongoni mwa miradi mikubwa iliyowahi kutekelezwa nchini, mradi wa  pamoja  baina ya Mashirika ya Kimataifa ya UN Women na UNFPA kupitia ufadhiri  wa  Shirika la KOICA wa Tuufikie usawa  wa jinsia kupitia kuwawezesha wanawake na wasichana utakaogharimu takribani bilioni 11.5 za kitanzania  ambao utatekelezwa  katika Wilaya...

WORLD VISION YAWANOA WANAHABARI KUHUSU LISHE NA AFYA YA UZAZI

Image
  Meneja wa Mradi wa ENRICH, Bi Mwivano Malimbwi (aliyesimama) akitoa mafunzo maalum ya malengo ya mradi huo ya utoaji wa elimu ya lishe na kuboresha afya ya uzazi kwa vijana balehe kwenye  mikoa ya Singida na Shinyanga kwa waandishi wa habari ya Mkoa wa Singida (hawapo pichani) leo, aliyekaa  ni mtaalam wa Jinsia na Utetezi wa Mradi Huo Tumaini Fred Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiangalia mazao ya asali na mashine ya kukamulia asali  ya kikundi cha ufugaji wa nyuki mkoani Singida kinachofadhiliwa wa World Vision hivi karibuni Na. John Mapepele ,Singida Shirika la World Vision nchini  limewataka waandishi wa habari kama wadau wakuu wa Shirika  hilo  kutoa taarifa sahihi za kazi za  shirika hilo  kwenye mradi wake wa ENRICH  ambao unatekelezwa  katika  mikoa ya Singida na Shinyanga. Mradi huo unalengo la kupeleka elimu ya lishe na afya ya uzazi kwa vijana balehe vijiji...